Friday, November 10, 2017

Hivi kweli Allah anajua maana ya neno “Israeli”?




Ibrahimu alimzaa Isaka.
Isaka alikuwa na wana wawili – Esau na Yakobo.

Kwa sababu ya  hila aliyofanyiwa Esau ya kunyang’anywa mbaraka, alikasirika sana akapanga kumwua Yakobo pale baba yao atakapokufa.

Imeandikwa katika Mwanzo 27:41


Esau akamchukia Yakobo kwa ajili ya ule mbaraka babaye aliombarikia. Esau akasema moyoni mwake, Siku za kumlilia baba yangu zinakaribia, ndipo nitakapomwua ndugu yangu Yakobo.

Ndio mama yao alipojua hayo, akamwambia Yakobo kimbia kwa mjomba wako Labani, kakae huko hadi hasira ya kaka itakapoisha. Huko akaenda kuishi kwa miaka 20.

Siku anarudi kwao, akiwa na wake, watoto na mali nyingi, ndipo usiku mmoja alipokutana na malaika wa Bwana aliyejigeuza kuwa binadamu; akimwakilisha Mungu. Wakashikana mieleka hadi asubuhi.

Ndipo yule aliyeshindana na Yakobo:

Akasema, Niache, niende, maana kunapambazuka. Akasema, Sikuachi, usiponibariki. Akamwuliza, Jina lako n'nani? Akasema, Yakobo. Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda. (Mwa 32:26-28)

 
Unaona sasa?
Yakobo akabadilishiwa jina. Akaitwa ISRAELI.
Maana yake nini?
MAANA UMESHINDANA NA MUNGU, NA WATU, NAWE UMESHINDA.

…………..
Sasa hebu ndugu mwislamu, nikuulize maswali machache:
1. Wewe mwislamu unakubali kuwa allah alishindwa na Yakobo?
2. Je, allah mwenyewe anakubali hilo?
3. Kama kweli allah anahusiana na Wayahudi, je, ni LINI alishindana na Yakobo na akashindwa?
4. Kama hakuwahi kushindwa na Yakobo, hilo jina alimpa la nini?
5. Je, allah anajua maana ya jina ISRAEL?
……………

Allah hana uhusiano WOWOTE na Yakobo wala Israeli.
Ni mtu tu kanakili mambo kutoka kwenye Biblia bila kujua hata maana yake na anataka kutuaminisha kuwa allah ana uhusiano na Israeli.

No comments:

Post a Comment