Friday, October 13, 2017

Je, ufalme ulitolewa Israeli wakapewa Waislamu?


 
Ulimwenguni kote ndugu zetu Waislamu wanadanganyana kuwa ufalme uliondolewa Israeli na wakapewa wao.
Inasikitisha na kutisha unapoona watu zaidi ya bilioni wakiamini UONGO 100%.
Acha tuingize hoja yao kwenye tanuru tuone kama itatoka bila kugeuka majivu na moshi.
Ndugu mwislamu, naamini unakubali kuwa ufalme lazima uwe na MFALME.


Siku moja Yesu aliingia Yerusalemu akiwa amepanda juu ya punda.
Na Mathayo anatuambia yafuatayo:
Haya yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema, Mwambieni binti Sayuni Tazama, MFALME WAKO anakuja kwako, Mpole, naye amepanda punda, Na mwana-punda, mtoto wa punda. (Mathayo 21:4-5)
Na kwa kuwa binti Sayuni (yaani Yerusalemu) alimkataa Mfalme wake, ndipo Mfalme huyo akamwambia binti Sayuni jambo:

Yesu akawaambia, Hamkupata kusoma katika maandiko, Jiwe walilolikataa waashi, Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni; Neno hili limetoka kwa Bwana, Nalo ni ajabu machoni petu?  KWA SABABU HIYO NAWAAMBIA, UFALME WA MUNGU UTAONDOLEWA KWENU, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake. (Mathayo 21:42-43)


Sasa kama wewe mwislamu unadhani “taifa jingine” ni wewe na umma wa Muhammad, hebu jibu maswali yafuatayo:
1. Je, kuna mahali popote ambapo Allah anakiri kuwa Yesu ni Mfalme?
2. Je, quran yako inamtambua wapi Yesu kuwa ni Mfalme?
3. Je, kuna mahali popote ambapo Muhammad anakiri kuwa Yesu ni Mfalme?
4. Je, wewe unamkiri Yesu kuwa ni Mfalme wako?
……………..
Kama majibu ya maswali hayo ni NDIYO, basi ni kweli “taifa jingine” ni wewe.
Kama majibu ni HAPANA, je, ni lini utaacha kujilisha uongo?

Yohana 8:12
Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye HATAKWENDA GIZANI KAMWE, bali atakuwa na nuru ya uzima.

Unaangamia.
Njoo nuruni.
Tafakari
Chukua hatua.

No comments:

Post a Comment